
by Dr. Respicius Kiiza
Fasihi kwa Ujumla Kidato cha Tano ni kitabu kinachoendana na Muhtasari Ulioboreshwa wa Elimu ya Sekondari, 2023 nchini Tanzania. Kutokana na mada zilizojadiliwa humu, kitabu hiki kitatumika kama kitabu cha ziada darasani kwa kidato kinachohusika. Upekee wa kitabu hiki ni kwamba, kimejadili mada zote zinazohusiana na fasihi kwa ujumla katika kidato cha tano. Mada zilizojadiliwa ni kama vile fasihi kwa ujumla (maana ya fasihi, sifa za fasihi, fasihi kama sanaa, aina za fasihi, dhima ya fasihi, na chimbuko la fasihi), maendeleo ya fasihi, kuhakiki kazi za fasihi pamoja na utungaji wa kazi za kifasihi.