
by Dr. Respicius Kiiza
Kitabu hiki kimeandikwa kwa kuzingatia matakwa ya mtaala ulioboreshwa na muhtasari wa somo la Historia ya Tanzania na Maadili wa mwaka 2023 wa shule za msingi nchini Tanzania. Kimeandaliwa ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi wa darasa la nne. Mada zilizomo zimejadiliwa kwa kuzingatia mazingira halisi ya utamaduni wa maisha ya Mtanzania.